• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Rais Dkt. Samia azindua Kiwanda cha Vioo Pwani

Posted on: September 21st, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua kiwanda cha kutengeneza vioo cha Sapphire Float Glass Tanzania Limited, kilichopo kijiji cha Mkiu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, ambacho ni kikubwa kwa ukanda wa nchi za Afrika Mashariki na kati lakini pia cha nne kwa nchi za Afrika.

Dkt. Samia amezindua kiwanda hicho leo Septemba 20, 2023 na kusema hatua hiyo ni mafanikio makubwa ya maboresho ya sera mbalimbali za uwekezaji ambazo zimesaidia kuwavutia wawekezaji.

Amesema hadi sasa kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha tani 750 za vioo kwa siku na kuajiri watu 1650 na kuongeza kuwa tayari soko la kuuza bidhaa hizo lipo nchini kwa asilimia 25 na 75 kikiuzwa nje ya nchi.

“Haya ndio matunda ya maboresho ya sera ya uwekezaji kwa kushirikiana na watalaam ambayo sasa tunaanza kuyaona, naamini nchi yetu itakuwa na wawekezaji wengi na tutafanya makubwa kwenye taifa hili kupitia sekta ya viwanda na biashara," amesema Rais Dkt. Samia.

Ameongeza kuwa katika kufanikisha hayo, Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na biashara imeandaa mfumo wa usajili kwa njia ya kielektroniki kwa wawekezaji ambapo watapata huduma za pamoja ikiwemo taratibu za upatikanaji hati za ardhi na leseni.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho, Zhen Yang amesema asilimia 80 ya malighafi yanayozalisha vioo hivyo yanapatikana nchini huku asilimia 20 pekee ndiyo kwa sasa yanatolewa nje ya nchi.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashantu Kijaji, amemuomba Rais Dkt. Samia kutoa kibali cha uchimbaji wa madini aina ya Soda Ash ambayo yanapatikana eneo la Engaruka mkoani Arusha ili malighafi zote za kutengeneza vioo yapatikane hapa nchini.

Amesema kupatikana kwa kibali na kuboreshwa kwa miundombinu ya eneo yalipo madini hayo ya Soda Ash huko Engaruka kutasaidia kupunguza gharama za wawekezaji hao kuyafuata nje ya nchi na kuisaidia serikali kuongeza mapato.

Katika hafla hiyo, Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amemueleza Rais, Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa mkoa huo una jumla ya viwanda 55 vilivyokamilika vinavyosubiri kuzinduliwa ili vianze kazi.

Kunenge amesema kuwa hadi leo, mkoa huo una viwanda 1525 ambapo kati yake vikubwa vikiwa 120 na vingine vikiwa ni vya kati na vidogo ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali na amewakaribisha wawekezaji kuendelea kuja kuwekeza kwa sababu fursa za uwekezaji katika mkoa huo bado zipo yakiwemo maeneo na mazingira yanavuyotia.

Ziara hiyo ya siku moja ya Rais Dkt. Samia mkoani humo pia imeshirikisha mawaziri mbalimbali na viongozi wa mkoa wa Pwani maalum kwa ajili ya uzinduzi wa kiwanda cha Sapphire Float Glass na kuzungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali mkoani humo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.