• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge Aagiza Kuandaliwa Shamba la Mfano kwa Wananchi

Posted on: October 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, ameagiza Idara ya Uzalishaji kumwandalia shamba la korosho ili aweze kulisafisha kama mfano kwa wananchi ambao hawasafishi mashamba yao, hali inayosababisha kupungua kwa uzalishaji wa zao hilo.

Agizo hili limetolewa lOktoba 10,2024, wakati wa mkutano wa wadau wa zao la korosho uliofanyika wilayani Mkuranga.

“Tunahitaji kuwa na uchungu na mashamba yetu ili kuongeza thamani na uzalishaji kwa ajili ya kukuza uchumi wetu. Ni kwa nini hatusafishi mashamba yetu? Na kwa nini hatupunguzi mikorosho mizee? Haya yote yanawezekana tukijipanga vizuri. Naagiza Mkuu wa Idara ya Uzalishaji anitayarishie shamba nitasafisha ili liwe mfano kwa wananchi,” alisema Mhe. Kunenge.

Aidha, Mhe. Kunenge aliagiza Bodi ya Korosho kuboresha zoezi la usajili wa wakulima ili kurahisisha utoaji wa pembejeo. Aliwataka wale wanaotoa taarifa zisizo sahihi kuchukuliwa hatua za kisheria. Alisisitiza kuwa majina ya wakulima yanapaswa kubandikwa kwenye mbao za ofisi za vijiji na vitongoji ili kuruhusu marekebisho ya taarifa kabla ya ugawaji wa pembejeo.

Pia aliwataka viongozi wa Vyama vya Msingi vya Awali (AMCOs) kutoa mrejesho kwa wananchi kuhusu makubaliano na maamuzi yaliyojadiliwa katika mkutano huo. Aliahidi kuandaa kikao na taasisi za kifedha ili kutatua changamoto ya wananchi kushindwa kupata mikopo na huduma za kifedha, jambo ambalo linachelewesha malipo kwa wakulima.

Mhe. Kunenge aliagiza mamlaka husika kuharakisha utoaji wa pembejeo kwa wakulima baada ya wadau kulalamikia ucheleweshwaji wa pembejeo, hali inayosababisha kupungua kwa uzalishaji wa korosho.

Aidha, alishukuru Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuimarisha mnyororo wa thamani wa zao la korosho kwa kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo kwa wakulima.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Bibi Hadija Nasri, alisema maendeleo ya zao la korosho yameimarika kutokana na maelekezo ya Mhe. Kunenge, na aliahidi kuwa maelekezo yote yaliyotolewa pamoja na michango ya wadau yatatekelezwa ipasavyo.

Kaimu Meneja wa Bodi ya Korosho, tawi la Dar es Salaam, Dominica Mkangara, alieleza kuwa wamejipanga kuajiri vijana kupitia mpango wa BBT kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) kwa ajili ya kusaidia zoezi la usajili wa wakulima.

Bodi ya Korosho pia ilishauri matumizi ya mizani ya kidigitali, ambapo Meneja Mkuu wa Ushirika CORECU, Hamisi Mantawela, alisema mkoa wa Pwani unahitaji mizani 188, na tayari mizani 135 imesambazwa kwa AMCOs zote 102 zinazohudumia wakulima wa korosho mkoani humo. Aliahidi kushirikiana na Korosho Cooperative Joint Enterprises Limited (KCJEL) ili kuhakikisha mizani iliyobaki inapatikana kwa wakati.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.