• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aelekeza matumizi Halmashauri Kuleta tija

Posted on: June 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amezielekeza Halmashauri za Mkoa huo kuzingatia matumizi ya mapato yenye kuleta tija kwa wananchi ili kuweza kukidhi matarajio yao ya kubadili hali za maisha yao kutoka kwenye uduni.

Kunenge ametoa maelekezo hayo leo Juni 19, 2024 alipokutana na kuzungumza na mabaraza ya maalum ya Rufiji na Kibiti yaliyokutana kwa nyakati tofauti kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali baada ya ukaguzi wa hesabu za fedha za mwaka 2022/2023 ulioishia juni 30, 2023.

Akiwa Rufiji kwenye Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, pamoja na kuipongeza halmashauri hiyo kupata hati safi, alisema wanaweza kuwa na hati safi lakini matumizi yao yasiwe na tija.

"Rufiji na halmashauri zingine zote za mkoa wa Pwani, hati safi sio 'issue' (suala) tena kwetu, sisi tunataka tija, hatuongelei tena hati safi, sisi tupo kwenye tija, kama wapo wanaopambana kupata hati safi, waache waendelee, sisi tunapambana na tija, amesema.

Katika mikutano hiyo, Kunenge ameyaelekeza mabaraza hayo kuhakikisha hoja zote zinapatiwa majibu na kuondolewa na kuepuka kuzalisha zingine mpya.

"Mwaka ujao kila mkuu wa Idara atakuwa anawasilisha hoja zake, awajibike nazo mbele ya kamati yako kwa sababu inaonekana wanapuuzia kuzishughulikia," ameagiza Kunenge.

Amewataka watendaji kuandaa mipango kazi ya kufunga hoja na maagizo ya Kamati ya Bunge na kuitekeleza huku akihadharisha wahusika wawe wanashughulikia mapema akisema "mtambue kuwa hoja zinazofika huku ni zile zinazokosa majibu ya ukaguzi toka kwa mkaguzi wa ndani ambazo kama mkizijibu hazifiki huku, zinazofika huku ni zinazoshindikana kufungwa na huo ni udhaifu ndani ya taasisi, na mtambue kuwa anaejibu si mkaguzi wa ndani, ni mkuu wa idara husika na timu yake ndani ya idara."

Katika mikutano hiyo Kunenge amesisitiza halmashauri kuongeza viwwngo vya mapato ili kuboresha huduma mwa wananchi, uzingatiaji wa Sheria, Taratibu na Kanuni pamoja na utekelezaji wa majukumu kwa umoja.

Mkuu huyo wa Mkoa pia ameupongeza uongozi na wakazi wa Rufiji na Kibiti kwa umoja, mshikamano na ushirikiano waliouonesha wakati wa changamoto ya Mafuriko yaliyoyakumba maeneo hayo mwanzoni mwa mwaka huu.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Skauti Mkuu wa Tanzania Rashid Mchatta amewapongeza na kuwashukuru wana Rufiji na Kibiti wa namna walivyopambana kudhibiti madhara na athari za changamoto za mafuriko pamoja na kwa kupata hati safi huku akizisisitiza halmashauri kujikita zaidi katika kutozalisha hoja za ukaguzi.

Awali, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rufiji Abdul Chobo amesema Halmashauri imepata hati safi baada ya ukaguzi wa hesabu za fedha za mwaka 2022/2023 ulioishia juni 30, 2023, Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali amejiridhisha kuwa kutokana na ushahidi wa vielelezo alivyopitia, Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji imepata hati safi.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ramadhani Shaha Mpendu ametoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa huduma wakati wa mafuriko na kwa kupatiwa fedha nyingi za miradi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.