• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

RC Kunenge ahimiza Ushirikiano Kati ya Serikali na Sekta Binasfi kukuza Biashara na Uwekazaji

Posted on: October 2nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.

Kunenge alitoa wito huo Oktoba 2, 2024 wakati wa kikao cha majadiliano kati ya sekta binafsi (PPD) na serikali kilichofanyika leo katika Ofisi za Mkoa wa Pwani.

Akizungumza katika kikao hicho, Kunenge alisema ushirikiano huo utawezesha kutambua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara, na hivyo serikali kuweza kuweka mazingira rafiki ya kukuza biashara na kuongeza uwekezaji.

"Lazima tushikamane kati ya sekta binafsi na serikali ili kuweza kujua wapi tunafanya vizuri na changamoto zilizopo ili kuhakikisha tunaboresha mazingira ya biashara na uwekezaji," alisema Kunenge.

Pia aliwataka wafanyabiashara kuhakikisha wanachangia kuongeza mapato ya serikali na kuboresha biashara zao kwa kutumia fursa mbalimbali zinazowezesha ukuaji wa biashara na uwekezaji kwa kufanya mambo tofauti na waliyozoea.

Aidha, Kunenge aliwaasa wafanyabiashara na wawekezaji kufuata matakwa ya kisheria ili kuweka mazingira bora yanayowezesha serikali kutoa msaada stahiki.

Alisisitiza maafisa biashara kufanya kazi kwa weledi ili kuleta matokeo chanya, akiongeza kuwa, "Tumia fursa unapopewa nafasi, na uhakikishe unachokifanya kinaonekana."

Kwa upande wake, Mwenyekiti (ni nani)wa Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani alishauri serikali kutoa elimu kwa walipa kodi kabla ya kuwakamata na kuwatoza faini, akisema kuwa hatua hiyo inachangia wafanyabiashara wengi kupoteza mitaji yao na kusababisha biashara zao kufa.

Alipendekeza pia serikali kutengeneza huduma wezeshi mkoani, kama vile masoko, ili kuvutia wafanyabiashara wengi zaidi.

Naye Mwenyekiti wa Jumuia ya Wafanyabiashara (JWT) Mkoa wa Pwani, Abdallah Ndauka, alitoa wito kwa maafisa biashara wa mkoa na halmashauri kuwasaidia wakurugenzi kutambua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara na kuziwasilisha kwa viongozi ili kuweka mazingira rafiki ya kutatua changamoto hizo na kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200