• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge Aitaka DAWASA Kufanya Tathmini Shirikishi ya Miradi ya Maji Kulingana na Mahitaji ya Wananchi.

Posted on: July 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kufanya tathmini ya kina ya utekelezaji wa miradi ya maji kwa kuzingatia changamoto halisi zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali.

Kunenge alitoa wito huo leo, Julai 2, 2025, wakati akifungua kikao kazi cha kupokea na kujadili mipango na mikakati ya DAWASA kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kilichofanyika katika ukumbi wa Destiny, Kibaha kwa Mathias, mkoani Pwani.

Amesisitiza kuwa tathmini yoyote ya miradi lazima itokane moja kwa moja na maoni ya wananchi pamoja na viongozi , badala ya kutegemea taarifa za ripoti peke yake ambazo mara nyingine hazioneshi uhalisia wa mambo.

“Tujitahidi kupata tathmini kutoka kwa wananchi na viongozi. Itakuwa ni jambo la kusikitisha kuwa na tathmini nzuri ilhali wananchi hawaridhishwi. Tathmini bora ni ile inayotoka kwa wananchi,” alisema Mhe. Kunenge.

Amesisitiza pia umuhimu wa kuwa na uelewa wa kina kuhusu hali ya upatikanaji wa maji kwa wananchi, na pale changamoto zinapotokea, hatua zichukuliwe kwa haraka. Aidha, alihimiza umuhimu wa kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu miradi inayoendelea ili kuepusha malalamiko au upotoshaji wa taarifa.

Kunenge aliitaka DAWASA kupanga vipaumbele vyenye uhalisia na vinavyotekelezeka, ili matokeo ya tathmini yawe na manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire, alisema kuwa kikao hicho kililenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa miradi na kuweka mikakati ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mchango wake mkubwa kupitia Programu ya “Kumtua Mama Ndoo Kichwani” iliyowezesha kupatikana kwa zaidi ya Shilingi Bilioni 220 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maji.

Akizungumzia maendeleo ya miradi ya maji mkoani Pwani, Mhandisi Bwire alieleza kuwa Mradi wa Maji wa Mkuranga I umekamilika, huku Mkuranga II ukiendelea kutekelezwa. Aidha, Mradi wa Kisarawe wenye thamani ya Shilingi Bilioni 10.6 unaendelea kukamilishwa.

Pia alibainisha kuwa utekelezaji wa Mradi wa Maji kutoka Bwawa la Kidunda umefikia asilimia 31, sambamba na maandalizi ya Mradi mkubwa wa maji kutoka Mto Rufiji, ambao unatarajiwa kuzalisha zaidi ya lita milioni 1.5 kwa siku – ukiwa suluhisho la muda mrefu kwa huduma ya maji katika Mkoa wa Pwani, hasa kutokana na ongezeko la viwanda na mahitaji ya maji.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, alipokuwa akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, aliipongeza DAWASA kwa juhudi zake katika kutekeleza miradi ya maji. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kufanya tathmini kwa kila mtumishi mmoja mmoja, ili kutambua changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa miradi na kuzitatua mapema.

Kwa sasa, Mkoa wa Pwani umefikia mafanikio makubwa katika huduma ya maji safi, ambapo upatikanaji mijini umefikia asilimia 93% na vijijini asilimia 83% – mafanikio yanayotokana na juhudi za Serikali kupitia DAWASA katika kuboresha maisha ya wananchi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Kikao Kazi cha Viongozi, Asisitiza Uboreshaji wa Vyanzo vya Mapato.

    July 15, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Pwani Akutana na Ujumbe wa NBC Kujadili Ushirikiano wa Kimaendeleo.

    July 15, 2025
  • Mnyema atoa wito wa Ushirikiano na Uwajibikaji kwa watumishi

    July 14, 2025
  • Waziri Mchengerwa aipongeza Shule ya Sekondari ya wavulana Kibaha kwa Ufaulu wa Kiwango cha Juu

    July 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.