• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge amshukuru Rais Samia kwa jitihada za kuboresha huduma za Afya

Posted on: September 18th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, ametoa shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kushirikiana na mataifa mbalimbali katika kutatua changamoto za afya nchini.

Kunenge aliyasema hayo leo wakati wa ziara ya Princess Sophia, mke wa mtoto wa Malkia wa Uingereza, alipotembelea mkoa wa Pwani kukagua maendeleo ya Mradi wa Macho. Mradi huu ni matokeo ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Uingereza katika kupambana na ugonjwa wa macho uitwao Trakoma.

"Namshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuleta mgeni huyu muhimu, ambaye amesaidia sana katika kuboresha huduma za afya," alisema Kunenge.

Katika ziara hiyo, Princess Sophia alitembelea Kituo cha Afya cha Mlandizi na kumtembelea Bibi Hadija Shabani, mkazi wa Kijiji cha Vikuruti, Wilaya ya Kibaha Vijijini. Bibi Hadija alikuwa muathirika wa ugonjwa wa Trakoma, lakini sasa amepona baada ya kufanyiwa upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mlandizi, ambako mradi huo wa macho umeanzishwa.

Serikali ya Tanzania, kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza, imefanikiwa kutoa msaada wa vifaa tiba, dawa, malipo ya mishahara ya madaktari, na kujenga chumba cha upasuaji cha kisasa katika Kituo cha Afya cha Mlandizi, Mkoa wa Pwani.

Kwa upande wake, Princess Sophia amepongeza jitihada za Serikali ya Tanzania na Uingereza katika kutokomeza ugonjwa wa Trakoma, na amewashukuru wahudumu wa afya kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuhudumia wananchi.

"Tunaishukuru Serikali ya Tanzania na Uingereza pamoja na wahudumu wa afya kwa huduma bora. Naamini, kwa jitihada hizi, tutafanikiwa kutokomeza kabisa ugonjwa wa Trakoma," alisema Princess Sophia.

Naye Waziri wa Afya, Jenista Mhagama, amewahimiza viongozi wa vijiji na vitongoji kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupata huduma za matibabu pindi wanapoona dalili za ugonjwa wa Trakoma, kwani kuchelewa kutibiwa kunaweza kusababisha upofu.

Aidha, alimtaka Bibi Hadija, ambaye amepona baada ya kufanyiwa upasuaji, kuwa mfano wa kuigwa kwa kuhamasisha watu wengine wanaosumbuliwa na ugonjwa huo kupata matibabu mapema.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.