• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aongoza Kikao cha Baraza la Biashara Mkoa na asisitiza kuongeza Uwekezaji na Ukusanyaji wa takwimu sahihi za Mapato

Posted on: May 22nd, 2025

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Mkoa huo, Mhe. Abubakar Kunenge, ameongoza kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kibaha, ambapo amesisitiza umuhimu wa kuzingatia dhana ya 4R ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili kuimarisha uwekezaji wenye tija utakaoleta maendeleo chanya kwa wananchi.

Mkutano huo umehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Katibu wa Baraza hilo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Dkt. Godwill Wanga, Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Mkoa wa Pwani (TCCIA), Bw. Saidi Mfinanga, pamoja na wakuu wa wilaya, wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, na wadau mbalimbali wa sekta binafsi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kunenge alieleza kuwa Mkoa wa Pwani unapaswa kuwa na mazingira bora ya kiuchumi yanayovutia wawekezaji, huku maendeleo yanayotokana na uwekezaji huo yakilenga kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla.

“Ili kufanikisha azma hii, Mkoa tayari umeanza utekelezaji wa mikakati kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, inayoongozwa na Prof. Kitila Mkumbo, kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo vinavyomilikiwa na wazawa,” alisema Mhe. Kunenge.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuweka na kuwasilisha taarifa sahihi za mapato kutoka viwandani, hasa vile vinavyokuwa kutoka hadhi ya viwanda vidogo hadi vikubwa, ili takwimu hizo zisomwe katika Mkoa wa Pwani na kuchangia kwa usahihi katika pato la taifa.

“Takwimu za pato la taifa kwa mkoa zinatokana na taarifa rasmi za mapato kuwasilishwa kwa mamlaka husika. Lakini kwa sasa hatufanyi hivyo. Viwanda vinakua kutoka vidogo hadi vikubwa lakini mapato yake hayaonekani yanasomeka nje ya Mkoa. Hili linaturudisha nyuma kimaendeleo,” aliongeza Kunenge.

Mhe. Kunenge pia alitoa agizo la kuanzishwa kwa mabaraza ya biashara hadi katika ngazi ya kata ili kuibua changamoto halisi zinazowakabili wafanyabiashara na wawekezaji, na kupanga mikakati sahihi ya kuzitatua. Aliwataka maafisa biashara kushirikiana kwa karibu na sekta binafsi ili kupata taarifa sahihi kuhusu maendeleo ya viwanda.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TNBC, Dkt. Godwill Wanga, alisisitiza umuhimu wa utoaji wa taarifa sahihi za uzalishaji kutoka kwa wawekezaji na wamiliki wa viwanda ili kusaidia Serikali kubaini fursa za maendeleo ya kiuchumi.

Dkt. Wanga pia alishauri Mkoa wa Pwani kuandaa mkakati maalum wa kuendeleza sekta ya utalii, akisisitiza kuwa mkoa huo una vivutio vingi vya asili ambavyo bado havijatumiwa ipasavyo kama chanzo cha mapato na ajira kwa wananchi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge aongoza Kikao cha Baraza la Biashara Mkoa na asisitiza kuongeza Uwekezaji na Ukusanyaji wa takwimu sahihi za Mapato

    May 22, 2025
  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.