• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aonya Viongozi wanaosababisha migogoro ya Ardhi

Posted on: August 11th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amesema hatowavumilia watendaji wa Serikali na chama ambao watabainika kuwa ndio chanzo cha migogoro ya ardhi katika kata ya Mapinga.

Mhe. Kunenge ameyasema hayo leo Agosti 10, 2022 wakati akipokea taarifa ya Kamati maalum iliyoundwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuchunguza mgogoro wa ardhi uliopo katika kata ya Mapinga Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo.

Kunenge amesema kuwa Serikali ya Mkoa haitamfumbia macho Mwananchi yeyote yule ambae nae atabainika kuwa ni chanzo cha mgogoro wa ardhi katika eneo hilo

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Kunenge amemuahidi Mhe. Mabula kuwa ataipitia kwa kina na wale wote ambao wametajwa kuwa ni chanzo cha mgogoro atahakikisha kuwa wanachukuliwa hatua za kisheria.

“Mhe. Waziri, nimepokea taarifa hii na naahidi kuwa nitaifanyia kazi na wale wote watakaobainika kuwa ni wahusika tutawachukulia hatua stahiki, hatutamuonea mtu wala hatutampendelea mtu tutatenda haki kwani hakuna aliye juu ya sheria,” alisema Mhe. Kunenge.

Pia ameeleza kuwa hata kama ni viongozi wa chama cha Mapinduzi wametajwa kuwa nao ni tatizo basi atashughulika nao kwa mujibu wa taratibu za chama.

Akikabidhi taarifa hiyo, Waziri wa Ardhi Nyumba Maendelo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula amesama kuwa lengo la kamati hiyo ni kutatua migogoro katika eneo hilo pia na sehemu nyingine nchini.

Amesema kuwa kamati hiyo imefanya kazi kwa umakini zaidi na kuwahoji watu mbalimbali ambapo wamebaini kuwa chanzo cha migogoro hiyo ni pamoja na wenyeviti wa vijiji na Vitongoji kuuza ardhi kiholela.

Waziri Mabula ametoa onyo kwa wenyeviti hao kuacha mara moja tabia ya kujipa madaraka ya kugawa ardhi bila ya kufuata sheria, kanuni na taratibu.

Mhe. Mabula alifafanua kuwa mkoa wa pwani ni Mkoa wa mfano kitaifa katika suala zima la uwekezaji na kwamba Mhe. Rais anautizama kwa macho mawili, hivyo ni lazima kumaliza migogoro yote ya ardhi katika mkoa huo ili uwekezaji usikwamishwe.

Aidha ameezielekeza Halmashauri zote nchini kuanza kufanya ukaguzi wa mashamba pori na orodha hiyo ikabidhiwe kwake kwani kuwepo kwa mashmba pori mengi nacho ni chanzo cha migogoro.

Pia ametoa rai kwa wananchi wote kuwa kama wanahitaji maeneo waende Halmashauri husika ambapo ndipo atapata eneo sahihi na si kwa wenyeviti wala Watendaji.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.