• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge atahadharisha Kongani SINOTAN Kutokwamishwa

Posted on: March 6th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge ameelekeza taasisi wezeshi Mkoani humo kuwa tayari mda wote kutatua changamoto zozote zinazoweza kujitokeza katika utekelezaji wa mradi wa Kongani ya SINOTAN iliyopo Wilayani Kibaha.

Kunenge alitoa maelekezo hayo leo Mach 6, 2023 alipotembelea na kukgua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kupokea maoni na mapendekezo ya mwekezaji ili kufanya maboresho yenye tija kwa pande zote mbili kwa maana ya Serikali na Mwekezaji

Akifafanua baadhi ya miradi inayotekelezwa na serikali kuwezesha Kongani hiyo ambayo aliitaja kuwa ni uwekezaji mkubwa mkoani humo itakayokuwa na viwanda zaidi ya 300 ambazo kwa pamoja zitatoa ajira 100,000, Kunenge alisema tayari Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoani humo wanatekeleza Mradi wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.3 ambao utakapokamilika utamaliza tatizo la uhaba wa maji hasa katika wakati huu wa Ujenzi na DAWASA wanajipanga kutekeleza mradi mkubwa utakao maliza tatizo la Maji katika eneo hilo na la Uwekezaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha huku TANESCO wakiboresha hali ya umeme kutoka Megawat 10 hadi 50 na kuwa kufikia mwezi Juni tatizo katika huduma hizo litakuwa limeisha.

Aliendelea kusema kuwa Serikali itakamilisha ujenzi na uwekaji wa miundombinu yote muhimu kwenye kongani ikiwa ni pamoja na barabara ya njia nne ya zege kutoka barabara kuu ya Dar es Salaam - Morogoro kupitia bandari kavu ya kwala hadi eneo la Kongani hiyo.

"Pwani tunaendelea kuwa mstari wa mbele kwa uwekezaji wa viwanda na mkoa huu ndio mfano mzuri, eneo hili litakuwa kubwa kwenye uwekezaji, wanaoanzisha Kongani kwenye maeneo mengine waje kujifunza hapa mpangilio na mambo mengine," alisema.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alieleza kuwa kufuatia mazungumzo ya pamoja na wataalamu kutoka kwenye taasisi wezeshi, kuanzia sasa watakuwa na utaratibu wa kukutana mara kwa mara kutatua vikwazo vinavyoweza kujitokeza kwenye mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.

"Tumekubaliana hizi taasisi zinazohusika na kuunganisha huduma kwenye hii kongani zikutane na uongozi wa SINOTAN ili waonyeshwe ramani ya mpango wa ujenzi, hii itasaidia kutoharibu maendelezo yaliyokamilika wakati wa kuweka miundombinu mingine na kupunguza gharama," alisema Kunenge.

"Lengo la Serikali chini ya Raisi Samia Suluhu Hassan ni kuwarahisishia wananchi maisha kwa njia mbalimbali ikiwemo kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa ajira hivyo kama viwanda hivyo vitaanza kazi nidhahiri vitakuwa vinajibu changamoto hizo," aliongeza.

Awali, Mwenyekiti wa Kongani hiyo Janson Huang alisema ifikapo June mwaka huu kituo cha huduma kitakuwa kimekamilika na kiwanda cha kwanza kitaanza kazi na kwa kuwa katika hatua za awali, takriban ajira 5000 zinatarajia kutolewa kwa watanzania.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.