• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge awataka maafisa Tarafa ,Watendaji Kata Pwani kutatua changamoto za Wananchi

Posted on: November 21st, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amewataka Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kutafuta majibu ya changamoto zinazowakabili wananchi kwa kuhakikisha wanakuwa wabunifu kwa kutumia rasilimali zilizopo kwenye maeneo yao.

Kunenge ameyasema hayo leo Novemba 20, 2023 akifungua mafunzo ya siku mbili kwa maafisa tarafa na watendaji wa kata 152 kati ya 160 wa Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani yanayofanyika katika kata ya Msangani Halmashauri ya Mji Kibaha.

Amesema mafunzo hayo yana tija kubwa kwa watumishi hao ambao moja kwa moja wanaishi na wananchi hivyo ni rahisi kufahamu vikwazo vinavyowakabili na kuwatatulia.

Kunenge ametumia nafasi hiyo kuwafundisha watumishi hao namna ya kuwa watumishi bora wenye kuzingatia sheria, kanuni za utumishi wa umma na akasema anaamini baada ya mafunzo hayo watafanya vizuri zaidi.

"Tunaishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa watumishi hawa kujengewa uwezo ili kuwa watumishi wanaotekeleza majukumu yao kwa weledi, nimekuwa nikitumia nafasi yangu kuwapa maarifa watumishi hawa kwa lengo la kujibu changamoto za wananchi kwa vitendo,” amesema.

Ameongeza kuwa anaamini baada ya mafunzo hayo wananchi watatatuliwa changamoto zao kwa wakati na kwa weledi unaotakiwa.

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Serikali za Mitaa, Ibrahim Minja amesema ni awamu ya pili mafunzo ya aina hiyo kutolewa ambao kwa sasa yanafanyika mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Mtwara, Singida, Dodoma na Tabora na kwa awamu ya kwanza yalitolewa mikoa ya Songwe, Njombe, Rukwa na Katavi.

Amesema mafunzo hayo yana mada 15 ambazo zitafundishwa na wataalam kutoka Chuo cha Hombolo na Utumishi wa Umma ambao watawafundisha namna ya kuzingatia misingi ya kazi ikiwemo la maadili ili kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Minja ameongeza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kupata matokeo mazuri ya kile walichokifundisha kwa wananchi ambao watafurahia huduma.

“Mafunzo haya yana lengo la watumishi hao kukumbushwa wajibu wao nafasi zao kufahamu miongozo mbalimbali ya utumishi ili kuboresha maisha ya watanzania,” amesema.

Baadhi ya washiriki katika mafunzo hayo akiwemo Jane Mwanantwa Afisa Mtendaji kata ya Kawawa wilaya ya Kibaha, amesema yana umuhimu kwa sababu wanakumbushwa wajibu wao pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo kukamilika kwa wakati pamoja na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wananchi wanaowahudumia.

Afisa Mtendaji wa kata ya Msangani, Benjamin Mputtu amesema wameongezewa maarifa ambayo yatawasaidia kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia sheria, kanuni taratibu na miongozo ya utumishi wa umma.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.