• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge azielekeza CMT kuongeza jitihada utekelezaji majukumu

Posted on: February 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amezisisitiza timu za Menejimenti za Halmashauri katika mkoa huo kusimamia ukusanyaji wa mapato kwa jithidada kubwa na kudhibiti mianya ya upotevu ili kuiwezesha serikali kutoa huduma kwa wananchi.

Kunenge ametoa msisitizo huo leo Februari 12, 2024 alipokutana na timu za menejimenti za halmashauri za Kibaha Mji, Kibaha DC, Bagamoyo na Chalinze ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI aliyeelekeza wakuu wa mikoa katika maeneo yao kukutana na timu hizo.

Maagizo ya Waziri wa TAMISEMI yameelekeza wakuu wa mikoa kufuatilia hali ya vipaumbele katika wakati huu wa maandalizi ya Mpango na bajeti ya 2024/2025 vinavyojibu hoja za wananchi, mikakati ya ukusanyaji mapato na udhibiti wa mianya ya upotevu wa mapato hayo.

Maagizo mengine yameelekeza halmashauri kutoa taarifa zao za upelekaji fedha zitokanazo na mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo, usimamizi miradi ili ikamilike kwa wakati na kwa ubora unaoakisi kiasi cha fedha kilichotolewa, taarifa ya utoaji wa asilimia 10 za mapato ya ndani kwa vijana, wanawake na wenye ulemavu pamoja na mikakati ya utekelezaji taarifa za hoja za Mdhibiti na Mkagunzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) na za Kamati ya Bunge LAAC na (TAMISEMI).

Katika mkutano wa kwanza kati yake na Menejimeti za Halmashauri za Kibaha TC na Kibaha DC kwenye ukumbi wa mikutano wa Kibaha TC na baadae za Bagamoyo na Chhalinze kwenye Ukumbi wa mikutano ofisi za halmashauri ya Bagamoyo, Kunenge amewaelekeza kufanya kazi kwa uwezo wao wote ili waweze kuleta matokeo chanya yenye kujibu changamoto za wananchi.

"Kila mtu atekeleze majukumu yake, tunatakiwa tukusanye mapato mengi zaidi kadri inavyowezekana ili tuweze kutoa huduma kwa wananchi ambao wanataka kila kitu cha kimaendeleo kinatekelezwa, tukijipanga vizuri tutafanikiwa kwani uwezo wetu ni mkubwa kuliko changamoto zinazotukabili," amesema.

Awali, Katibu Tawala Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Skauti Mkuu wa Tanzania Rshid Mchatta ameeleza kuwa tayari ameshafanya kikao na wakurugenzi wote wa halmashauri mkoani humo kuweka mikakati ya pamoja itakayoweza kufanikisha utoaji bora huduma kutokana na kuongeza jitihada kuharakisha maendeleo kwa kuboresha ukusanyaji mapato na kuweka mifumo mizuri ya usimamizi wa maelekezo ya serikali.

Nazo Menejimenti hizo zimeahidi kuwasilisha mikakati yao ya utekelezaji wa maelekezo hayo kikamilifu

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.