• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

SALFA YA WIZI YAKAMATWA WILAYANI MKURANGA.

Posted on: September 12th, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imekamata salfa ya wizi mifuko 247 yenye thamani ya Tshs 6,916,000 katika kijiji cha Msonga ikiwa katika maandalizi ya kuanza kuuzwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filberto Sanga akizungumza mbele ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na baadhi ya watendaji na wataalam mbalimbali alisema ”Siku ya alhamisi ya tarehe 3/08/2017 usiku walibaini kuna salfa nyumbani kwa mwananchi mmoja hivyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi salfa hizo zilikamatwa na kuhifadhiwa zikisubiri upelelezi ukamilike”.

Mhe. Sanga alisema kuwa baada ya upelelezi kukamilika salfa hizo zitagawiwa kwa wananchi wa Mkuranga kama salfa za awali zilivyogawiwa.

Aidha Mhe. Sanga ametoa wito kwa watendaji wote wa Serikali kuwa waaminifu na kuacha ubadhilifu na udanganyifu katika mali za umma.

Mhe. Sanga alisema Wilaya ya Mkuranga ilipokea pembejeo za ruzuku kwa asilimia mia moja za korosho, kiasi cha kilo 453,875 sawa na mifuko 18,155 ya salfa ya unga katika awamu 4, yaani mifuko 8,314, mifuko 5,998, mifuko 2,390 na mifuko 1200. Pia jumla ya lita 6,886 za salfa ya maji, lita 1,231 dawa za wadudu na mabomba 41.

Kupitia kamati ya pembejeo ya Wilaya, mgao wa pembejeo hizo ulifanyika kwa kila Kijiji kwa kutumia kigezo cha idadi ya mikorosho.

Mhe. Sanga alisema pamoja na mafanikio ya ugawaji wa pembejeo hizo kuna changamoto zilizojitokeza ikiwemo udanganyifu kwa upande wa wakulima kwa kutoa takwimu za uongo juu ya idadi ya mikorosho waliyonayo kwa lengo la kupatiwa mgao mkubwa wa pembejeo. Vilevile pembejeo kutotosheleza mahitaji halisi kwa wakulima kwani kuna upungufu wa takribani tani 346 za salfa ya unga, lita 7,000 za salfa ya maji, lita 3,000 za dawa za wadudu na mabomba 85. Pia changamoto kwa baadhi ya Watendaji wa Vijiji kutowasilisha takwimu za mikorosho kwa Vijiji vyao mfano Kijiji cha Marogoro kata ya Vianzi na kusababisha wakulima wa maeneo hayo kukosa pembejeo.

Akizungumza namna ya kutatua changamoto hizo Mhe. Sanga alisema mpaka sasa Wilaya imepeleka maombi ya kupatiwa nyongeza ya pembejeo na imefanikiwa kupatiwa tani 10 zaidi za salfa ya unga lakini pia Watendaji wameelimishwa juu ya ukusanyaji wa takwimu sahihi za mikorosho kutoka kwa wakulima japo takwimu hizi hazikuweza kutumika tena msimu huu bali zitatumika kwa msimu ujao.

Mhe. Sanga alisema wakulima wengi wamehamasika kusafisha mashamba yao hasa baada ya kuambiwa kigezo kimojawapo cha kupatiwa pembejeo ni kuwa na shamba la mikorosho lililopaliliwa, vilevile Wilaya imeweza kupata takwimu za awali za idadi ya mikorosho waliyonayo wakulima. Hii itasaidia kutathmini mahitaji halisi ya pembejeo.

Bi. Julita Bulali - Afisa kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Wilaya ya Mkuranga alisema kumekuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa takwimu sahihi kutokana na wakulima kutokuwa na ushirikiano, hivyo katika harakati za kupambana na changamoto hiyo viongozi wa Vijiji wakiwemo Wenyeviti wa Vitongoji wameagizwa kubainisha idadi ya mikorosho.

Wilaya ya Mkuranga ni miongoni mwa Wilaya zinazolima korosho na kwa Mkoa wa Pwani inaongoza kwa kuwa na takribani mikorosho milioni tatu na inazalisha wastani wa tani 9,000 kwa mwaka.

Katika msimu wa 2016/2017 wilaya imeuza korosho kiasi cha kilo 6,647,081 na kuingiza jumla ya Tshs 15,846,498,022.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.