• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Timu ya Michezo ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani yashiriki Uzinduzi wa Mashindano ya 39 ya SHIMIWI.

Posted on: September 7th, 2025

Timu ya michezo ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani imeshiriki katika uzinduzi wa Mashindano ya 39 ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), yaliyofanyika leo, tarehe 07 Septemba 2025, katika Uwanja wa CCM Kirumba, Wilaya ya Ilemela, mkoani Mwanza.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, ambaye aliwataka washiriki wa mashindano hayo kuyachukulia kama fursa ya kujenga afya bora ili kuweza kutoa huduma nzuri na bora kwa wananchi.

Aidha, aliwataka viongozi wa SHIMIWI kuhakikisha kuwa wanaratibu mazoezi ya awali kwa wachezaji ili kuwaandaa kiakili na kimwili, pamoja na kuhakikisha upimaji wa afya unafanyika kwa kushirikiana na taasisi za afya nchini ili kupata wachezaji wenye afya bora na kuepuka matukio ya maradhi ya ghafla wakati wa mashindano.

Mhe. Dkt. Biteko alibainisha kuwa tasnia ya burudani, ambayo michezo ni sehemu yake, inaendelea kukua kwa kasi na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa na kuongeza ajira. Alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2022/23 sekta hiyo ilikua kwa asilimia 15, huku mwaka wa 2023/24 ikikua kwa asilimia 18.

Aliongeza kuwa watumishi wa umma nchini ni sehemu muhimu ya maendeleo ya sekta ya michezo kupitia SHIMIWI, kwani wamekuwa wakikusanya maelfu ya wachezaji wanaoshindana na kuonyesha ari ya kimashindano, hivyo kuchochea jamii kuthamini michezo na kuwahamasisha vijana kushiriki kikamilifu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, akitoa salamu za mkoa, aliishukuru Serikali kwa kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha michezo kwa kuwekeza katika miradi mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Kulea Vipaji katika Chuo cha Michezo Malya kwa zaidi ya shilingi bilioni 31.

Aidha, Mhe. Mtanda alitumia fursa hiyo kuwaalika tena SHIMIWI na mashirikisho mengine ya michezo kufanya mashindano yao mkoani Mwanza, akisisitiza kuwa mkoa huo una miundombinu rafiki ya viwanja, malazi, vivutio vya utalii, na maeneo safi ya kupumzika, hasa katika fukwe za Ziwa Victoria.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Gerson Msigwa, alieleza kuwa mashindano hayo hayajawahi kusimama kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo. Aliahidi kuwa wizara itaendelea kuyasimamia kwa kuhakikisha yanakuwa ya haki na mshindi anapatikana kwa njia halali.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Pwani Yatenga Maeneo 27 ya Kongani Kukuza Uwekezaji na Viwanda.

    September 11, 2025
  • Lishe Bora Chachu ya Maendeleo - RC Pwani.

    September 09, 2025
  • Pwani Kunufaika na Vyandarua Milioni 1.2 Kukabili Malaria.

    September 09, 2025
  • Timu ya Michezo ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani yashiriki Uzinduzi wa Mashindano ya 39 ya SHIMIWI.

    September 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.