• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ulega awaasa wafugaji kuanzisha vyama vya Ushirika

Posted on: August 26th, 2024

Ulega awasa wafugaji kuanzisha vyama vya Ushirika.

Waziri wa Mifugo na maendeleo ya Uvuvi Abdalla Ulega amewaasa wafugaji nchini kuanzisha na kujiunga na vyama vya Ushirika ili kupata tija katika uzalishaji, utunzaji na uuzaji mazao yatokanayo na mifugo ndani na nje ya nchi.

Aliyasema hayo alipotembelea na kukagua Machinjio ya "Union Meat Abattoir Ltd." yaliyopo kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani ambapo ameeleza kuwa Ushirika utawapa wafugaji manufaa ya kuinua na kuimarisha uchumi wa mfugaji mmoja mmoja na Taifa Kwa Ujumla.

Kufuatia ombi la Kampuni inayomiliki Machinjio hayo ya kupewa maeneo ya kukusanya na kulisha mifugo kabla ya kuingizwa machinjioni, Waziri Ulega ameiagiza kampuni ya Ranchi za Taifa Ltd (NARCO) kutenga eneo Kwa ajili hiyo na kuikabidhi kwa Kampuni hiyo mapema iwezekanavyo.

"Ninatambua maombi yenu ya kupatiwa eneo, ninaielekeza NARCO itoe eneo hilo haraka iwezekanavyo, apewe mwekezaji kabla ya msimu wa mvua ili aandae na kupanda malisho tayari kwa kupokea mifugo, mkataba na makabidhiano yakamilike mara moja ndani ya mwezi huu wa tisa kwani huu sio wakati wa danadana, ni wakati wa kuamua," amesema Ulega.

Pia waziri huyo kupitia machinjio hayo amewaasa vijana wanaopata ajira kwenye maeneo ya uwekezaji kufanya kazi kwa uadilifu, uaminifu na bidii kubwa na kuepuka wizi huku akihimiza muwekezaji wa machinjio hayo kuweka viwango vizuri (gharama za huduma na bei za bidhaa) ili waweze kuwavutia wafanya biashara wengi zaidi wafikishe mifugo yao kuchinjwa hapo.

Mkurugenzi Mtendaji wa machinjio hayo Mariam Ng'wandu amesema wametumia Dola za kimarekani Milioni kumi (sawa na shilingi bilioni 26 za kitanzania) kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wake na wa Zahanati ya Kijiji cha Vigwaza na kwamba kitakamilika kwa ujenzi wa awamu tatu.

Naye mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Pwani ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon amesema kuwa Serikali imeweka miundombinu wezeshi na rafiki Kwa wawekezaji kama vile huduma za maji, umeme na Barabara ili kurahisisha uwekazaji.

Akiwa katika Kata ya Kwala Kijiji cha Mperamumbi kitongoji cha Msua Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Waziri Ulega amepata fursa ya kujionea uwekezaji wa uchimbaji wa bwawa la kunyweshea mifugo.

Hadi sasa ujenzi wa Bwawa hilo umegharimu kiasi cha shilingi milini 75.23, fedha hizo ni zilizochangwa na wafugaji ambao walitoa kiasi cha shilingi milioni 63.76, mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha shilingi milioni 10 na wadau mbalimbali shilingi milioni 1.51.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.