• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Utekelezaji TIRP2 wa TRC unamanufaa kwa jamii - Nsajigwa.

Posted on: July 17th, 2025

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Nsajigwa Geoge ameeleza kuwa Serikali imefanya jambo kubwa na lenye tija kuanzisha mradi wa ukarabati wa reli ya kati wa awamu ya Pili kutoka Dar es Salaam hadi Isaka, mkoani Shinyanga (TIRP2).

Nsajigwa ameyasema hayo leo Julai 17, 2025 baada ya kupokea taarifa ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) iliyowasilishwa kwake na ujumbe wa shirika hilo uliyoongozwa na Mhandisi Dkt. Veronica Mirambo kwa lengo la kutambulisha mradi huo ambao unatarajiwa kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani na Taifa kwa ujumla.

“Mradi huu ni wa manufaa makubwa kwa wananchi. Mbali na kuimarisha usafiri wa abiria na mizigo, pia utaongeza fursa za ajira kwa wananchi wa kada mbalimbali wakati wa utekelezaji wake,” alisema Nsajigwa.

Aidha Aliahidi ushirikiano wa karibu kutoka kwa uongozi wa mkoa ili kuhakikisha kuwa shughuli zote za utekelezaji wa mradi zinafanyika kwa ufanisi.

Akiwasilisha taarifa ya shirika hilo, Mhandisi Dkt. Veronica Mirambo ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Mazingira na Jamii kutoka TRC alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo una ushirikiano kati ya TRC na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kufadhiliwa na Banki ya Dunia.

Alisema kwa sasa wako katika hatua za awali za kuanza utekelezaji wa Mradi huo ambapo timu ya wataalamu inatembelea maeneo yote yatakayohusika na ukarabati huo, ikiwa mkoa wa Pwani ni moja kati ya maeneo hayo.

Alisema lengo kuu la ukarabati wa reli hiyo ni kuboresha usalama, kuongeza ufanisi katika usafiri wa reli, pamoja na kuhakikisha miundombinu inakuwa imara na endelevu kwa kuzingatia athari za mabadiliko ya tabianchi katika kipindi chote cha uendeshaji.

Akibaninisha malengo mahususi kadhaa ya Mradi ni kuboresha njia ya reli na madaraja, kujenga mabwawa ya kupokea maji ya mvua ili kupunguza madhara ya mafuriko, na kuongeza uwezo wa kusafirisha abiria na mizigo ndani ya nchi na nje ya mipaka, hususan kuelekea nchi jirani.

Mradi huu pia utahusisha kuimarisha uwezo wa taasisi zinazohusika kama TRC, NIRC, LATRA pamoja na Wizara husika. Sambamba na hilo, mradi unalenga kuweka mazingira rafiki kwa sekta binafsi kushiriki katika kutoa huduma za reli kupitia mfumo wa uwekezaji huria (open access).

Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuleta fursa mbalimbali kwa wananchi, ikiwemo ajira kwa watu wenye ujuzi na wasiokuwa na ujuzi, kukuza biashara katika maeneo yanayopitiwa na reli, kurahisisha usafiri wa abiria na usafirishaji wa mizigo, na hivyo kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Vilevile, kupitia mabwawa yatakayojengwa, mradi huu utawawezesha wakulima kupata maji ya umwagiliaji, pamoja na wafugaji kupata maji kwa ajili ya mifugo yao, hatua ambayo inatarajiwa kusaidia kuboresha maisha ya jamii katika maeneo yanayopitiwa na mradi.

Shirika la Reli Tanzania linaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau mbalimbali kuhakikisha utekelezaji wa mradi huu unazingatia viwango vya kimataifa na unawanufaisha Watanzania kwa kiwango cha juu.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Ufunguzi wa Kikao cha Mpango wa MTAKUWWA II.

    July 18, 2025
  • Utekelezaji TIRP2 wa TRC unamanufaa kwa jamii - Nsajigwa.

    July 17, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Kikao Kazi cha Viongozi, Asisitiza Uboreshaji wa Vyanzo vya Mapato.

    July 15, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Pwani Akutana na Ujumbe wa NBC Kujadili Ushirikiano wa Kimaendeleo.

    July 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.