• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wakuu wa mikoa watakaowasilisha Bajeti bila ya kutenga asilimia kumi bajeti zao hazitapitishwa -Jafo

Posted on: March 11th, 2020

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo,amewatahadharisha Wakuu wa Mikoa nchini ambao watawasilisha bajeti zao bila kutenga asilimia 10 kwa mujibu wa Sheria na kwamba bajeti zao hazitapitishwa.

Jafo alitoa angalizo hilo jana Mjini Kibaha alipokuwa katika kikao Cha kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Pwani ambacho kilijadili mpango wa bajeti ya mwaka 2020/2021 kwa Mkoa huo.

“Mkoa wowote, Mkuu wake wa Mkoa akileta taarifa ya mapendekezo ya mpango wa bajeti haitajadiliwa katika kikao cha kamati ya bajeti endapo haitaonyesha asilimia 10 iliyotengwa kwa mujibu wa Sheria" alisema.

Alisema kwenye taarifa ya bajeti kila mkuu wa mkoa atatakiwa kuwa na jedwali linaloonyesha namna Halmashauri zinavyotoa asilimia kumi kwa ajili ya mikopo ya makundi ya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu

Aidha alisema, hatakubaliana na Mkuu wa mkoa yeyote ambaye atakwamisha bajeti kwenye Wizara ya Tamisemi badala yake atapeleka majina kwa Rais kumueleza watu wanaokwamisha bajeti katika Ofisi yake.

Akizungumzia suala la ukusanyaji wa mapato Jafo alisema, Mkoa wa Pwani bado hali hairidhishi kutokana na Halmashauri mbili pekee kati ya tisa ndizo zinazofanyika vizuri.

Kufuatia hali hiyo ametoa agizo kwa Wakurugenzi kuhakikisha wanasimamia fedha zinazokusanywa kuingizwa katika mfumo wa Serikali.

Jafo alisema, mashine nyingi za kukusanyia fedha bado zinachezewa na kusababisha makusanyo yanayopatikana kutoingizwa katika mfumo wa Serikali.

Katika hatua nyingine Jafo alitoa maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya zote nchini kuainisha maeneo ambayo yameathiriwa na mvua zinazonyesha na kusababisha baadhi ya shule kufungwa.

Waziri Jafo alisema, ni vema maeneo hayo yakajulikana ili wanafunzi wanaosoma katika shule hizo watafutiwe mbadala waendelee na masomo hususani wale ambao wanamitihani ya kitaifa.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, alisisitiza kila Halmashauri kusimamia ukusanyaji wa mapato kupitia vyanzo vya ndani.

Kikao hicho kilipitisha mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2020/2021 Shilingi Bilion 251.57.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.