• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wananchi wa Pwani Wahimizwa kutunza Mazingira

Posted on: June 7th, 2018

Wananchi Mkoani Pwani wametakiwa kutumia nishati mbadala badala ya mkaa ili kuweza kupunguza uharibu wa mazingira unaosababishwa na matumizi makubwa ya mkaa.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo mwanzoni mwa wiki hii katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani .

Pia amewapongeza wananchi hao kwa juhudi za uhifadhi wa mazingira katika upandaji na utunzaji wa miti, ambapo jumla ya miti 7,716,819 imepandwa.

Mhandisi Ndikilo alisema kuwa utunzaji wa misitu unafaida kubwa ,kwani ni moja ya rasilimali inayoweza kuzuia mabadiliko  ya tabia  ya Nchi.

“Tukiharibu mazingira maana yake ni kwamba tunajiletea matatizo makubwa sana yakiwemo athari za mafuriko,kuongezeka kwa joto, kuongezeka kwa kina cha bahari pamoja na magonjwa mbalimbali na kukauka  kwa vyanzo vya maji”alisema Ndikilo.

Aidha  mhandisi Ndikilo alisema kuwa Suala la utunzaji wa mazingira  linakumbwa na changamoto nyingi ikiwemo uvunaji ovyo wa misitu,kilimo kisichozingatia  kanuni bora za kilimo, kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji na uchimbaji holela wa mchanga katika kingo za mito.

Katika Hatua nyingine Mhandisi Ndikilo amepiga marufuku uchimbaji holela wa mchanga  na ameagiza ifanyike tathimni ya mazingira ndipo leseni ya uchimbaji mchanga itolewe.

“Maelekezo ya Serikali ya Mkoa ili tuweze kupambana na uchimbaji holela wa mchanga katika Mkoa wetu wa Pwani hasa katika Wilaya za Mkuranga,Kibaha na Bagamoyo ni lazima sasa kabla kuchimba mchanga kwanza tathmini ya mazingira ifanyike  vizuri ndipo leseni ya uchimbaji wa mchanga itolewe na mashimo yote yanayoendelea kuchimbwa sasa hivi maelekezo ya Serikali ya mkoa  ni lazima Idara ya mazingira  ngazi ya Halmashuri na ngazi ya Mkoa waendelee kuyafuatilia maeneo hayo ili kuona kuwa yako salama kwa ajili ya binadamu kwenye maeneo husika”alisema Ndikilo.

Maadhimisho ya kilele cha siku ya Mazinga Duniani kitaifa yalifanyika Mkoani Dar es Salaam na kwa Mkoa Pwani maadhimisho hayo yalifanyika Wilayani Mkuranga katika Kijiji cha Kisemvule yakiwa na kauli mbiu ya Mkaa ni gharama,tumia nishati Mbadala.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.