• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wavamizi hifadhi ya Mikoko Bagamoyo Watii agizo la Kuhama

Posted on: June 7th, 2023

Wakazi wa Changwahela ‘A’ Wilayani Bagamoyo wameitikia agizo la kutekeleza maelekezo ya Serikali la kuondoka katika eneo walilolivamia na kufanya shughuli za kibinadamu zenye uharibifu wa Mazingira.

Hali hiyo inafuatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ambaye ameiagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS, Mkoa wa Pwani kusimamia uhifadhi wa miti ya mikoko na kuzuia uharibifu wa mazingira uliofanywa na wananchi wa kitongoji cha Changwahela ‘A’ kilichopo Mapinga ambao wameamriwa kuondoka mara moja.

Kunenge alitoa agizo hilo wakati alipofika na kuzungumza na wananchi wa kitongoji cha Changwahela ‘A’leo Juni 7, 2023 katika kushughulikia changamoto zinazotokana na migogoro ya ardhi.

Akiwa katika eneo hilo, Kunenge amesema kuwa kuna uharibifu mkubwa umefanywa na wananchi hao ikiwamo ukataji hovyo wa mikoko ambayo inatunza kingo za bahari na kuhifadhi mazingira ya fukwe.

Amefafanua kuwa maagizo hayo ni utekelezaji wa maamuzi yaliyofanywa na baraza la Mawaziri kufuatia ushauri wa timu ya mawaziri wanane wa kisekta iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mwaka 2019/2020 ambao walishirikiana wataalamu kushughulikia migogoro ya ardhi mkoani humu na maeneo mengi nchini.

Kutokana na maamuzi hayo, Kunenge amemuagiza Kamishna wa Ardhi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kukaa na mwekezaji anayemiliki kiwanda cha Sea Salt na eneo lenye ukubwa wa ekari 600 ili waweze kumega ekari 50 n kuwapatia wananchi wa Changwahela ‘A’ ambao wametakiwa kuondoka eneo la mikoko.

“Nawaagiza TFS, kuanzia sasa simamieni eneo hili ambalo limeharibiwa na wananchi kutokana na shughuli za kibinadamu zinazofanywa kama vile uvuvi ambao umeharibu mikoko yetu na ujenzi wa nyumba 90 ambazo pia hazitakiwi kuwepo hapa hakikisheni uoto wa asili ulioharibiwa unarejea,” amesema Kunenge.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Changwahela, Kulwa Isdory amesema wamelipokea kwa mikono miwili agizo hilo na wapo tayari kuhama na kwenda eneo ambalo serikali imependekeza kuanza maisha mapya.

Akiwa Wilayani Bagamoyo, mkuu huyo wa mkoa pia alifika katika mtaa wa Sanzari Kata ya Magomeni na kuwaelekeza wakazi waliyovamia eneo la Yusuph Kikwete kupisha ili mwenyewe aweze kuendelea na shughuli za uwekezaji au wakae nae na kukubaliana watakavyoona inafaa.

Wakati huo huo, Kunenge ametoa muda wa siku 90 kwa Halmashauri ya Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo kukamilisha zoezi la urasimishaji makazi kwa ajili ya mpango wa matumizi ya ardhi kwa wananchi wa waliopewa eneo la ekari 5520 za Ranchi ya Taifa ya Ruvu.

Kunenge ametoa kauli hiyo alipozungumza na wananchi wa kata ya Vigwaza kwenye mkutano wa hadhara, amedai kuwa zoezi hilo la urasimishaji makazi utavihusu vijiji 11.

Ameyataka maeneo ambayo yanahitaji urasimishaji kuwa ni Ruvu- Darajani- Bagamoyo ekari 500, Miro ekari 1000, Vigwaza ekari 20, Kidomole 100, Mkenge 100, Fukayosi 100, Kitonga 1200, Waja 1500 na Maguri 500.

“Baada ya kukamilisha taratibu zote kumega maeneo ya ranchi ya Ruvu nimetoa siku 90 kwa uongozi wa Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo kushughulikia ili wananchi wapate maeneo yao ambayo yametolewa na serikali, sitarajii kuona uvamizi wa maeneo mengine sasa,” amesema Kunenge.

Ziara ya leo ya Mkuu huyo wa Mkoa ni muendelezo wa utekelezaji wa mpango wake wa kushughulikia kero za wananchi zinazotokana na migogoro ya ardhi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.