• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wawekezaji Kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira ni Muhuimu-Rc Ndikilo

Posted on: February 17th, 2021

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarisrt Ndsikilo amewataka wawekezaji Mkoani humo kuzingatia athari za uchafuzi wa Mazingira kabla ya kuanzisha Viwanda. “Uanzishwaji wa Viwanda katika Mkoa wa Pwani lazima uendane pia na masuala ya Mazingira. Tathimini ya Athari ya Mazingira ni muhimu” Ameyasema hayo Februari 16,2021 wakati wa ziara ya Mhe. Ummy Mwalimu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Wilayani Kibaha.

Ndikilo Amewataka pia Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira NEMC kutoa kwa wakati vyeti vya athari za mazingira ili wawekezaji wasikwame katika uwekezaji “Viwanda vingine vinashindwa kuanzishwa kwa wakati kwa kukosa cheti cha Tathimini ya Mazingira EIA Certificate’ tufanye haraka ili tusikwamishe wawekezaji ambao wapo tayari kutuletea ajira”

Amezungumzia pia uthibiti wa Taka kutoka kwenye Viwanda, Ni kweli tumetenga maeneo ya Viwanda, lakini viwanda vingine vipo kwenye maeneo ya watu. Ametaka Wizara kuangalia namna nzuri ya kutatua changamoto hii kwa viwanda ambavyo tayari vimejengwa kwenye maeneo ya watu kuliko kufunga viwanda hivyo jambo ambalo ni hasara kubwa kwa wawekezaji.

Amesema Mkoa huo unakabiliana na changamoto uchimbaji holela wa mchanga na ukataji wa misitu ovyo. Wanachimba mchanga kwenye maeneo yetu vijijini mwishoe wanaondoka na kuachia vijiji mashimo na mabwawa.“Mhe Waziri hawa waliopewa vibali vya kuchimba mchanga Pwani wadhibitiwe na sheria ili wasiache mahandaki kwenye maeneo hayo” alisitiza Ndikilo. Ameeleza pia suala la ulinzi wa vyanzo vya maji bado ni changamoto sheria ipo Mita 60 kutoka katika mto lakini Maeneo ya Mto Ruvu na Wami bado yamevamiwa.amewataka wanachi waachane na tabia hiyo na kufuata sheria inavyotaka.

Ametaja pia hatua iliyopigwa na Halmashauri za Mkoa katika kudhibiti taka ngumu, tumejitahidi lakini bado wasafiri wa mabasi wanatupa taka ngumu hovyo.” Tushirikiane na wizara kuazisha vikundi na kutoza adhabu ndogo ndogo ili kudhibiti tabia hii. Ndikilo Ameethibitisha kuwa Agizo Makamu wa Rais la kufanya Usafi la kila Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi linatekelezwa vizuri kwa wananchi kushiriki ipasavyo kwenye maeneo yao.

Mhe Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Ummy Mwalimu ameupongeza Mkoa huo kwa utendaji kazi na kumhakishia Mkuu wa Mkoa kuwa NEMC itaondoa changamoto ya ucheleweshaji wa vibali tathmini ya mazingira na kuacha mara moja tabia ya kuwakamata na kuwatoza faini ovyo wawekezaji

“Nilishawaambia NEMC msifanye kazi ya polisi ya kufunga kiwanda na kutoza faini. Mkiona kiwanda kinachangamoto nendeni mkakae na mmiliki wa na muone namna ya kuzitatua”alisema Mhe Ummy.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.