• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Waziri Mkuu Majaliwa aridhishwa na Maendeleo ya Ujenzi wa reli ya Kisasa(SGR

Posted on: May 15th, 2020

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na kazi ya ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salam Morogoro ambayo imefikia asilimia 77.91.

Majaliwa alibainisha hayo jana alipokuwa akiongea katika kituo cha soga Wilayani Kibaha wakati alipotembelea maendeleo ya mradi huo

Alisema kuwa kampuni ya Yap Merkezi imefanya kazi kama walivyosaini kwenye Mkataba na Serikali na naamini watakamilisha kazi kabla ya muda.

Waziri Mkuu huyo alisema, reli hiyo itatembezwa na umeme kutoka katika chanzo cha Kidatu Morogoro, Bwawa la Mwalimu Nyerere Rufiji pamoja na Kinyerezi ambacho kitakuwa kinatumia gesi.

" Reli haitasimama kwa kukosa umeme, mbali ya vyanzo hivi vitatu pia mabehewa yatakuwa na uwezo wa kutunza umeme kwa dakika 45 ikitokea ukakatika kwenye vyanzo vyote Jambo ambalo hatutarajii litokee" alisema Majaliwa.

Akizungumzia ajira kwenye ujenzi huo alisema, katika eneo la Dar es Salam Morogoro ajira 7400 zilitolewa na Morogoro Makutupora watu 6300 walinufaika na ajira.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema, ni matarajio ya Serikali ifikapo mwezi Mei 2021 reli hiyo ianze kufanya kazi, ambapo inadaiwa treni ya abiria itakiwa na uwezo wa kubeba abiria 560 hadi 600.

Katika hatua nyingine Majaliwa amewataka wananchi kuchukua taadhaali na kufuata maelekezo ya wataalamu ili kujikinga na virusi vya Corona kwani hakuna dawa ambayo imepatikana hadi sasa.

Nae Naibu Waziri Ujenzi na Mawasiliano Atashasta Nditie alisema kuwa lengo la ziara hiyo ya Waziri Mkuu ni kuangalia maendeleo ya mradi huo na utayari wake wa kuanza kazi katika kipindi Cha miezi miwili ijayo.

Nditie alisema, kuna vitu vidogo vilibakia ambavyo vilisimama kutokana na hali ya mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini.

Alisema reli hiyo ya kisasa itakapokamilika wananchi watafanya safari kwa haraka na ambapo kutoka Dar es Salam hadi Morogoro itakuwa kwa muda ea saa 1.30.

Aidha Naibu Waziri huyo alisema, treni hiyo ya kisasa ina faida za kiusalama kwani kila itakapokuwa inajulikana maeneo yote inayopitia.

Mkurugenzi wa Shirika la Reli Masanja Kadogosa alisema kuwa ,gharama ya ujenzi wa mradi huo wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salam hadi Makutopora Singida utagharimu kiasi cha Shilingi trilion 7 hadi kukamilika.

Kadogosa alisema, hadi sasa ujenzi wa reli hiyo kutoka Dar es Salam hadi Morogoro kwa urefu wa kilomita 300 umekamilika kwa asilimia 77.9.

Mkurugenzi huyo alisema, mvua zinazoendelea kunyesha hapa chini zilikwamisha baadhi ya kazi kukamilika kwa wakati.

Meneja Mradi msaidizi Mhandisi Ayoub Mdachi alisema,treni ya mizigo itakuwa na uwezo was kubeba tani 10,000 kwa mara moja, na itakuwa na uwezo was kutembea kilometa 120 kwa saa wakati treni ya abiria ikitembea kilomita 160 kwa saa.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.