• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Dkt Magere apongeza usimamizi mradi wa Umeme JNHP Rufiji

Posted on: July 22nd, 2020

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Dkt Delphine Magere ameipongeza timu ya wataalamu wakitanzania wanaosimamia ujenzi wa mradi wa bwawa litakalotumika kuzalisha umeme wa maji la Julius Nyerere (JNHPP-MW2115) kwa jinsi wanavyojituma kutekeleza majukumu yao.

Dkt.Magere alitoa pongezi hizo alipofanya ziara kujionea hali ya maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo ambalo hadi sasa ujenzi wake unaendelea kwa kasi.

”Tumekuta mradi ukiendelea vizuri kutokana na usimamizi mzuri wa wataalamu weenyeji, tumeiona faida ya kazi kusimamiwa na weenyeji, huu ni mmoja kati ya miradi michache inayosimamiwa na watanzania na inaendelea vizuri, ninawapongeza sana” alisema Dkt. Magere.

Katika ziara hiyo, Dkt. Magere alishuhudia na kupata maelezo ya kazi za ujenzi wa handaki la kuchepusha maji (diversion tunnel), tuta kuu (main dam), kingo ndogo za kuzuia maji (saddle dams), jengo la mitambo (power house), mitambo ya kuzalisha umeme (electromechanical Equipment), kituo cha kupokea na kusafirisha umeme (400kV switchyard) na daraja la kudumu (permanent bridge),

Kazi zingine katika mradi huo ni za ujenzi wa barabara za kudumu (Permanent roads), nyumba za makazi 113 (employee’s operation village), uchimbaji na uimarishaji wa kingo pamoja na ujenzi wa njia ya kupeleka maji katika mtambo (water way).

Dkt. Magere alitoa wito kwa halmashauri za Wilaya zinazopitiwa na mradi huo kuwa na ubunifu wa kuandaa mazingira mazuri yatakayosaidia kutunza vifaa vya utekelezaji wa mradi huo na kujiongezea mapato ya ndani kutokana na shughuli mbalimbali zinazohitaji gharama.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi Mushubila Kamuhabwa alieleza kuwa tayari watanzania wameanza kufaidika nao katika hatua za awali kwa kupata ajira ambapo tayari wameajiriwa wafanyakazi 4,027 kati ya wafanyakazi 6,000 wanaohitajika na wengi wao wakiwa ni weenyeji wa vijiji vya maeneo ya jirani kama Mloka na Kisaki.

Mhandisi Mushubila aliongeza kuwa mradi huo pia umechochea matumizi ya bidhaa na huduma mbalimbali za hapa nchini kuweza kununuliwa na kutumiwa kwenye ujenzi huo.

“Makampuni na viwanda vya ndani vinauza bidhaa zao hapa na mfano ni saruji tani 850,000, nondo tani 70,000 pazolana tani 250,000 inanunuliwa kutoka kwa watoa huduma wa hapa hapa nchini ili kuchochea ukuaji wa uchumi wetu” alisema Mhandisi Mushubila.

Akifafanua manufaa ya mradi huo utakapokamilika, Mhamdisi Mushubila alisema kuwa utadhibiti mafuriko kwenye maeneo ya ukanda wa chini ya bwawa, utawezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika na wa gharama nafuu, utasaidia kuongeza ujuzi na uzoefu kwa wataalamu wa ndani katika kujenga na kusimamia miradi kama hiyo, kutakuwa na ongezeko la mapato ya TANESCO kwa uuzaji wa umeme utakaozalishwa kwa gharama nafuu, ongezeko la mapato ya serikali yatakayotokana na tozo mablimbali, ongezeko la upatikanaji wa maji kwa matumizi ya binadamu na wanyama na uvuvi endelevu katika bwawa la mradi.

Alifafanua manufaa mengine kuwa ni kuanzisha aina mpya ya utalii wa majini, manufaa katika ekolojia, kuanzisha kilimo cha umwagiliaji katika eneo lenye ukubwa wa takriban hekta 1,500,000, kuzipatia soko bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani na kuongeza ajira.


Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.