• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Makamu wa Rais awahimiza Wananchi kushiriki Uchaguzi kwa Amani

Posted on: April 2nd, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa amani na utulivu ili kuhakikisha wanapata viongozi bora.

Dkt. Mpango alitoa rai hiyo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2025, zilizofanyika katika viwanja vya Shirika la Elimu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.

“Kama kauli mbiu yetu inavyosema, mwaka huu, 'Shiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.' Tujitokeze kwa wingi katika kutumia haki yetu ya msingi na kuchagua viongozi wetu kwa amani na utulivu,” alisema Dkt. Mpango.

Aliongeza kuwa serikali itaendelea kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafanyika kwa uhuru na haki, ili kuwawezesha wananchi kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.

Aidha, aliwasisitiza wakimbiza Mwenge wa Uhuru kukagua miradi kwa ustadi na kutokusita kufichua ubadhilifu wa mali, fedha, pamoja na wala rushwa bila woga.

Awali, akimkaribisha Makamu wa Rais kuzindua Mwenge wa Uhuru, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema aliridhishwa na maandalizi ya sherehe hizo na kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe Abubakar Kunenge pamoja na Kamati ya Maandalizi. Waziri Mkuu aliongeza kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika mikoa 31 na kukagua miradi 195.

Pia alisisitiza Amani na Utulivu, kama kaulimbiu inavyosema, ni muhimu katika kuendeleza juhudi za Serikali katika kukuza uchumi wa nchi. "Amani na utulivu ndio msingi wa maendeleo yetu, bila Amani na utulivu hakuna maendeleo," alisisitiza Mhe. Majaliwa.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete, alisema kuwa katika kipindi chote cha mbio hizo, Mwenge wa Uhuru utahimiza wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “Jitokeze Kushiriki Katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.”

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amesema utakimbiza katika Halmashauri zote tisa na Wilaya saba za Mkoa wa Pwani mwenge na utapitia na kukagua miradi 64 yenye thamani ya shilingi trilioni 1.028.

Mara baada ya kuzinduliwa, Mwenge wa Uhuru umeanza mbio zake katika Mkoa wa Pwani, ukikimbizwa katika Manispaa ya Kibaha.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.