• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

MRADI WA KUZALISHA UMEME STIEGLER’S GORGE HYDROPOWER DAM WATARAJIWA KUWA MUARUBAINI WA UPUNGUFU WA UMEME -RC NDIKILO

Posted on: September 16th, 2017

Wakazi wa Wilaya ya Rufiji, Mkoani Pwani pamoja na watanzania kwa ujumla wanatarajia kunufaika na mradi mkubwa wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge Hydropower Dam Project), ambao utakuwa na uwezo wa kuzalisha megawatts 2,100. Mradi huo utazalishwa kutoka chanzo hicho , katika pori la akiba la Selous kanda ya kaskazini (Matambwe). Kwasasa nchi inazalisha megawatts 1,450 lakini Stiegler’s gorge itazalisha megawatts 2,100 hali itakayoleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi .

Akizungumza mara baada ya kwenda kukagua na kujiridhisha eneo utakapozalishwa mradi huo kabla ya utekelezaji kuanza, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist W. Ndikilo, alisema tangazo rasmi limeshatolewa na Wizara ya Nishati na Madini tangu mwezi tarehe 30/08/2017. Aidha alifafanua kuwa, tangazo hilo linawapa nafasi kwa makampuni ya ujenzi wa mabwawa ya maji ya kuzalisha umeme.

Mhandisi Ndikilo, alibainisha kampuni yoyote iwe ya ndani ama nje ya nchi ikikidhi vigezo itatangazwa. Alieleza endapo mradi utakamilika utawezesha kuwepo kwa umeme wa uhakika na kuvutia wawekezaji kwa wingi. Wilaya ya Kisarawe na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Kibiti na Rufiji kuna changamoto ya upungufu wa umeme hali inayokwamisha jitihada za kuinua sekta ya uwekezaji na viwanda .

“Tatizo la umeme bado ni kubwa Mkoani hapa licha ya Mkoa huu kusheheni viwanda “Mradi umekuja muda muafaka ambapo Mkoa huo umejipanga kuwa ukanda wa viwanda ” alifafanua.

Aidha Mh.Ndikillo alisema kwamba mradi umekuja muda muafaka na umefika mahala pake , ambapo Mkoa huo umejipanga kuwa ukanda wa viwanda .

“Ni nia ya Serikali ya awamu ya tano kuhakikisha mawazo ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ya tangu mwaka 1980 juu ya kuzalisha umeme kutoka katika maporomoko ya mto huo yanatekelezwa kwa haraka iwezekanavyo “ alisema mhandisi Ndikilo .

Baada ya kutembelea eneo la mradi Mhe. Ndikilo, alipata fursa ya kwenda kuzungumza na wakazi wa Kijiji cha Mloka kilicho mpakani mwa pori la akiba la Selous. Hata hivyo Mhe. Ndikilo, alisema kuwa ujenzi wa mradi huo utafungua milango ya kiuchumi, ujasiriamali na kibiashara.

Eneo litakalotumika kujenga mradi ni kilometa za mraba 1,350 ambalo ni sawa na asilimia tatu pekee ya eneo lote la pori la akiba la Selous yenye ukubwa wa kilometa za mraba 50,000.

Mkuu wa pori hilo kanda ya kaskazini (Matambwe) Bw. Lawrence Okode, alisema katika historia jina la Stiegler’s Gorge limetokana na Mjerumani aliyefariki katika eneo hilo aliyejulikana kwa jina la Stiegler’s baada ya boti yake kugonga jiwe kubwa na kusababisha umauti wake .

Kwa upande wa wakazi wa Mloka, Ikwiriri na Kibiti waliridhia na kuonyesha kukubali maendeleo wanayosogezewa. Mkazi wa Mloka Mzee Mbonde, alisema alikuwepo enzi za Hayati Baba wa Taifa wakati mradi ulipofanyiwa tathmini na watu wa Norway. Mzee Mbonde na Bibi Fatuma Majengo walimpongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya. Walisema kwa mwanzo huu, Mhe. Magufuli atatatua tatizo la uhaba wa umeme.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.