• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenenge Mapato hayana mipaka ya kiutawala

Posted on: June 24th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amezielekeza halmashauri za mkoa huo kumaliza migogoro ya ardhi ili kuwezesha kuongeza kasi ya uchumi kukua na kupanuka hali itakayoziwezesha kuongeza mapato yao.

Kunenge ameyasema hayo kwa nyakati tofauti kwenye vikao vya mabaraza ya Halmashauri ya Kibaha Mji na Bagamoyo kujadili hoja za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali vilivyofanyika kwenye kumbi za halmashauri hizo Juni 24, 2024.

Amezieleza halmashauri hizo kuwa Bila kumaliza migogoro ya ardhi hawawezi kuwa na maeneo ya kufanyia shughuli za kiuchumi na hivyo kuzorotesha maendeleo ya wananchi.

"Mapato yanatengenezwa, yanakusanywa na kupangiwa matumizi kwenye maeneo yenye vipaumbele, mapato ni akili, tengeneza mapato mwenyewe hivyo bila kumaliza migogoro ya ardhi hauna maeneo ya kufanyia shughuli za uchumi," amesema.

Kuhusu hali ya halmashauri hizo kufanikiwa kufikia au kuvuka lengo la asilimia za ukusanyaji wa mapato, Kunenge amewaasa kutoridhika na hali hiyo kwa kuwa bado kuna mahitaji makubwa ya huduma kwa wananchi kwani kila mwaka malengo yanaongezeka kutokana na idadi ya watu kuongezeka.

"Watoto wanazidi kuzaliwa, kuna mahitaji kama madarasa, vituo vya kutolea huduma za afya, mahitaji ya maji, miundombinu, haya yote yanahitaji mapato hivyo wekeni jitihada na mikakati ya kuongeza ukusanyaji.

Alihoji kwanini halmashauri zinakuwa na tofauti ya makusanyo na halamashauri zingine kwa kufuata mipaka ya kiutawala huku zikiwa na fursa lukuki akisema, "hakuna laana ya makusanyo ya mapato yanayozingatia mipaka, mnapakana na halmashauri zenye mapato makubwa, kwanini nyie mkusanye kidogo?" amehoji Kunenge.

Katika mikutano hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Skauti Mkuu wa Tanzania Rashid Mchatta mbali na kuzipongeza halmshauri hizo kwa kupata hati safi na kwa kuvuka lengo la makusanyo, amezielekeza kumaliza hoja zilizobaki.

Mchatta pia amezelekeza halmashauri hizo kutekeleza maagizo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kutumia vitendea kazi kama vile vishikwambi na matumizi ya mifumo kama ule wa e-office na mingine ili kuondokana na matumizi ya karatasi.

Naye Mkaguzi wa nje Mkoa wa Pwani toka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi CPA Pastory Masawe amezipongeza halmashauri hizo kupata hati safi na akazitahadharisha kutobweteka na kuharibu hiyo sifa ambayo kwa halamashauri ya Kibaha Mji imeendelea kuwepo tangu ianzishwe.

Na amewaasa kuendelea kufanya maboresho kwenye makusanyo na matumizi.

"Kuna maeneo ambayo ni pamoja na ukusnyaji na kusimamia mapato, kukusanya ni jambo moja lakini kutumia pia ni jambo lingine, kile tunachokikusanya tujaribu kukitumia vizuri," amesema.








Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.