• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Watumishi wa Umma na sekta binafsi Mkoani Pwani watakiwa kutimiza wajibu wao

Posted on: August 21st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewaagiza watumishi wa Umma na sekta binafsi mkoani humo kila mmoja kutimiza wajibu wake katika kuwatumikia wananchi ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili kwa wakati.

Ndikilo alitoa agizo hilo  mjini Kisarawe akiwa katika mkutano na wakazi wa mji huo, katika ziara yake ya kikazi kusikiliza kero za wananchi anahoifanya Mkoani humo akiambatana na kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa, pamoja na wayendaji.

"Tusisubiri viongozi wa ngazi ya kitaifa wafike kutatua kero za wananchi kwenye vitongoji na kata hii si sawa, jipangeni kuwasikiliza wananchi na kutafuta ufumbuzi wa vikwazo vya maendeleo kwao na pia mnapotatua kero jaribuni kutumia mbinu tofauti" alisema.

Mhandisi Ndikilo alisema, kila mmoja anatakiwa kusimama katika nafasi yake kuhakikisha hakuna kero ambayo iko ndani ya uwezo wake na haijapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

" Wananchi leteni taarifa kama kuna mtumishi wa mkoa ambaye hawajibiki ipasavyo kwenye eneo lake, huu sio wakati wa kuendelea kuwavumilia watu ambao hawawajibiki katika nafasi zao" alisisitiza Ndikilo.

Katibu Tawala wa mkoa huo Dkt Delphine Magare alisema hatakuwa tayari kumvumilia mtendaji ambaye hatatekeleza ipasavyo majukumu yake na kwamba yeyote atakayeenda kinyume atamchukulia hatua za kinidham .

Awali akiongea katika mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo aliwataka watendaji kufanya kazi na kumsaidia Rais John Magufuli badala ya kuwa mzigo na kushindwa kutekeleza majukumu yao kama inavyotakiwa.

" Wataalamu wafanye kazi zao mambo mengi wanaweza kuyamaliza kabla hayajafika mbali, wazitendee haki dhamana zao, wasilundike kero za wananchi na kugeuka kuwa mizigo kwa kushindwa kusimamia nafasi zao" alisema.

Katika mkutano huo wananchi wengi walilalamikia suala la fidia ambalo alielekeza idara husika kulitafutia ufumbuzi wa haraka.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.